Tuesday, October 29, 2019

Ni kwanini Kanisa katoliki limewaruhusu wanaume waliooa kuwa mapadri?


papa
Maaskofu wa kanisa katoliki wamepiga kura kuruhusu wanaume waliooa kuwa mapadri katika eneo moja la pembezoni ili kuweza kupata mwanya wa kuhubiri katika eneo la Amazon.
Hatua hiyo imekuja mara baada ya Papa Francis kutoa ombi kuwa ni vyema kutoa ruhusa kwa wanaume walioa kuwa mapadri kwenye sehemu maalum katika eneo hilola Amazon.
Eneo ambalo waumini wengi wanaotaka kushiriki misa na kupokea mkate wa komunio hawaonagi mapadri kwa zaidi ya miezi kadhaa na muda mwingine hata miaka.
Amesema yeye na washiriki wengine wanaojulikana kama 'synod' wapo wazi kwa mawazo ya kutafuta njia mpya itakayosaidia kusambaza imani hiyo.
Watahitajika kupata wanaume wanaoheshimika na kulingana na stakhabadhi hizo watafanya kazi katika jamii wanazotoka.
Maaskofu wa Marekani Kusini wamepigania juhudi hizo ili kukabiliana na upungufu wa mapadri katika eneo hilo.
mapadreHaki miliki ya pichaAFP
Lakini wakosoaji wamedai kuwa papa anapaswa kuhamasisha mapadri wasioe, ingawaje katika karne ya kwanza ya kanisa, mapadri waliruhusiwa kuoa, na karibia mapapa wote wa mwanzo walikuwa wameoa.
Vilevile kuruhusu wanaume walioa katika sehemu za Amazon ambazo zinakabiliana na ukosefu wa mapadri, kutaenda kinyume na sheria za kikatoliki ambazo zimekuwepo kwa miaka kadhaa sasa.
Kwa sasa papa anaruhusu wanaume walioa kuwa mapadri katika makanisa ya mashariki ya kati pekee.
Deacons like Shainkiam Yampik Wananch minister to Catholics in the Peruvian AmazonHaki miliki ya picha
Upigaji kura ukiwa unafikia ukingoni huko Vatican kutokana na uhaba wa mapadre ili mapendekezo hayo yaanze kufanya kazi rasmi.
Wengi wakiwa wanahofia mabadiliko hayo katika kanisa kwa kuanzisha utaratibu mpya katika kanisa.
Kura zimechukuliwa kwa kipindi cha wiki tatu,kwa maaskofu 180 wa mjini Rome.
Wakiwa wanaangalia majukumu ya wanawake katika kanisa na namna mazingira yatakavyoweza ruhusu.
Kanisa katoliki ni taasisi kongwe ya kidini ambayo imekuwa na historia kwa zaidi ya miaka 2000 iliyopita huku ikiwa na mabilioni ya waumini.
Huku inakadiriwa kuwa karibu 85% ya vijiji huko Amazon haviwezi kusherehekea Misa kila wiki kwa sababu ya uhaba huu na wengine huonana na makuhani mara moja tu kwa mwaka.

Related Posts:

  • Rwanda yazindua magari rafiki kwa mazingira Rwanda ikishirikiana na kampuni ya Volkswagen na Siemens imezindua magari ya kwanza ya umeme nchini humo yatakayokuwa rafiki kwa mazingira . Mradi huo ulioanza na magari 50 ambayo yametengenezwa kwa ajili ya majaribio hi… Read More
  • Pirates kidnap nine from Norwegian ship off Benin Image copyrightImage captionThe Benin navy's anti-piracy team on patrol in the Bight of Benin in the Gulf of Guinea Pirates have kidnapped nine crew members from a Norwegian shipping vessel off the coast of Benin in West A… Read More
  • American football coach is suspended after team scores too much Image copyrightImage captionThe coach will be absent from the sidelines of his team's game on Saturday (stock photo) A Long Island football coach has been reprimanded after his team thrashed another high school 61-13 in a … Read More
  • BE PATIENT Be Patient and Trust the Process! 👇🏽 An elephant and a dog became pregnant at same time. Three months down the line the dog gave birth to six puppies. Six months later the dog was pregnant again, and nine months … Read More
  • Ni kwanini Kanisa katoliki limewaruhusu wanaume waliooa kuwa mapadri? Maaskofu wa kanisa katoliki wamepiga kura kuruhusu wanaume waliooa kuwa mapadri katika eneo moja la pembezoni ili kuweza kupata mwanya wa kuhubiri katika eneo la Amazon. Hatua hiyo imekuja mara baada ya Papa Francis ku… Read More

0 comments:

Post a Comment