Wednesday, October 30, 2019

BE PATIENT

Be Patient and Trust the Process! 👇🏽 An elephant and a dog became pregnant at same time. Three months down the line the dog gave birth to six puppies. Six months later the dog was pregnant again, and nine months on it gave birth to another dozen puppies. The pattern continued. On the eighteenth month the dog approached the elephant questioning, _"Are you sure that you are pregnant? We became pregnant on the same date, I have given birth three times to a dozen puppies and they are now grown to become big dogs, yet you are still pregnant. Whats going on?". The elephant replied, _"There is something I want you to understand. What I am carrying is not a puppy but an elephant. I only give birth to one in two years. When my baby hits the ground, the earth feels it. When my baby crosses the road, human beings stop and watch in admiration, what I carry draws attention. So what I'm carrying is mighty and great.". Don't lose faith when you see others achieving their success. Don't be envious of others results. If you haven't received your success, don't despair. Say to yourself "My time is coming, and when it hits the surface of the earth, people shall yield in admiration.
.

Tuesday, October 29, 2019

Ni kwanini Kanisa katoliki limewaruhusu wanaume waliooa kuwa mapadri?


papa
Maaskofu wa kanisa katoliki wamepiga kura kuruhusu wanaume waliooa kuwa mapadri katika eneo moja la pembezoni ili kuweza kupata mwanya wa kuhubiri katika eneo la Amazon.
Hatua hiyo imekuja mara baada ya Papa Francis kutoa ombi kuwa ni vyema kutoa ruhusa kwa wanaume walioa kuwa mapadri kwenye sehemu maalum katika eneo hilola Amazon.
Eneo ambalo waumini wengi wanaotaka kushiriki misa na kupokea mkate wa komunio hawaonagi mapadri kwa zaidi ya miezi kadhaa na muda mwingine hata miaka.
Amesema yeye na washiriki wengine wanaojulikana kama 'synod' wapo wazi kwa mawazo ya kutafuta njia mpya itakayosaidia kusambaza imani hiyo.
Watahitajika kupata wanaume wanaoheshimika na kulingana na stakhabadhi hizo watafanya kazi katika jamii wanazotoka.
Maaskofu wa Marekani Kusini wamepigania juhudi hizo ili kukabiliana na upungufu wa mapadri katika eneo hilo.
mapadreHaki miliki ya pichaAFP
Lakini wakosoaji wamedai kuwa papa anapaswa kuhamasisha mapadri wasioe, ingawaje katika karne ya kwanza ya kanisa, mapadri waliruhusiwa kuoa, na karibia mapapa wote wa mwanzo walikuwa wameoa.
Vilevile kuruhusu wanaume walioa katika sehemu za Amazon ambazo zinakabiliana na ukosefu wa mapadri, kutaenda kinyume na sheria za kikatoliki ambazo zimekuwepo kwa miaka kadhaa sasa.
Kwa sasa papa anaruhusu wanaume walioa kuwa mapadri katika makanisa ya mashariki ya kati pekee.
Deacons like Shainkiam Yampik Wananch minister to Catholics in the Peruvian AmazonHaki miliki ya picha
Upigaji kura ukiwa unafikia ukingoni huko Vatican kutokana na uhaba wa mapadre ili mapendekezo hayo yaanze kufanya kazi rasmi.
Wengi wakiwa wanahofia mabadiliko hayo katika kanisa kwa kuanzisha utaratibu mpya katika kanisa.
Kura zimechukuliwa kwa kipindi cha wiki tatu,kwa maaskofu 180 wa mjini Rome.
Wakiwa wanaangalia majukumu ya wanawake katika kanisa na namna mazingira yatakavyoweza ruhusu.
Kanisa katoliki ni taasisi kongwe ya kidini ambayo imekuwa na historia kwa zaidi ya miaka 2000 iliyopita huku ikiwa na mabilioni ya waumini.
Huku inakadiriwa kuwa karibu 85% ya vijiji huko Amazon haviwezi kusherehekea Misa kila wiki kwa sababu ya uhaba huu na wengine huonana na makuhani mara moja tu kwa mwaka.

Rwanda yazindua magari rafiki kwa mazingira


Rwanda ikishirikiana Kampuni ya Volkswagen na Siemens imezindua magari ya kwanza ya umeme
Rwanda ikishirikiana na kampuni ya Volkswagen na Siemens imezindua magari ya kwanza ya umeme nchini humo yatakayokuwa rafiki kwa mazingira .
Mradi huo ulioanza na magari 50 ambayo yametengenezwa kwa ajili ya majaribio hivyo yatakuwa yakitumiwa kama magari ya uchukuzi wa abiria jijini Kigali na kwingineko nchini humo.
Mkurugenzi mkuu wa Volkswagen Group ya Afrika kusini, Thomas Schäfer amebainisha kuwa magari haya yamo bado katika majaribio na kwamba yametengenezwa 40 aina ya e.Golf na kwamba malengo kwanza si kuuzwa ghali ingawa bei bado haijatangazwa.
''Magari haya hayana mpango wa kuuzwa kwa wateja kwa sasa. Tunalenga kwanza kuyafanyia majaribio na kujua yanafanya kazi vipi na ndipo tutakapowajulisha iwapo zitauzwa au la. Magari haya ni ghali ikilinganishwa na yale ya kawaida, kutokana na betri yake.
Betri peke yake ina gharimu kiasi cha dola 8000 za Kimarekani lakini umeme ukilinganishwa na mafuta ni bei nafuu.
Lakini iwapo serikali ikiwasaidia kwa kuweka sera mfano kwa kupata faida nafuu ,yamkini hali ikawa nzuri zaidi.
Angalia Uchina serikali iliazimia kwamba asilimia 25 ya magari yanayouzwa yawe yanayotumia umeme.''
Magari ya umeme
Serge Iyakoze ni kiongozi wa madereva wa kampuni ya Valkswagen akihusika pia kutoa warsha kwa madereva wenza katika matumizi ta teknolojia ya magari hayo ambaye ameiambia BBC kuhusu wasiwasi au hofu kuhusu mwendo wa kimya wa magari hayo na iwapo hawatarajii kusababisha ajali za barabarani kwa watu waliozoea milio na honi za magari kuwashtua wanaotembea kwa miguu.
''Unapoelekea kupata ajali kawaida huna budi kupiga honi kwani dereva ana uwezo kuangalia kwa upana mkubwa mbele yake,kwa muda mfupi.
Dereva huwa na hisia za kujua kinachoelekea kutokea kwa wakati mfupi. Unapomuona mtu akizubaa unaweza kumpigia honi. Lakini huwezi kwenda ukipiga honi ovyo ovyo,kwani hata mpita njia anao uwezo kuona gari na unaweza pia kumwashia mataa.''
Kampuni imeeleza kuwa inalenga kupanua wigo wa kazi zake katika mataifa mengi ya Afrika .
Baada ya Rwanda, Ghana ndiyo inatarajia kufuata na hatimae kwingineko.
Wakati mataifa ya Ulaya yanalenga kufikia mwaka 2030 kuwa yamekwisha achana na magari yanayotumia mafuta, Afrika ndiyo imeanza safari ambayo hatima yake haijawa wazi ila waliozungumza na BBC wameelezea kuwa hatimae wao pia watafika.

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA


Baghdadi akihutubia wafuasi wake mjini Mosul mwaka 2014Haki miliki ya picha
Image caption
Vikosi vya muungano vya Syria (SDF) vinavyoongozwa na wapiganaji wa Kikurdi vinasema majasusi waliiba nguo za ndani za Abu Bakr al-Baghdadi ambayo ilitumiwa kufanya uchunguzi wa chembe chembe za vinasaba, DNA kabla auawe.
Kamanda wa mwandamizi wa SDF Polat Can anadai kuwa wapelelezi wao walichangia kwa kiasi kikubwa juhudi za kupata maficho ya kiongozi wa kundi la Islamic State (IS) kabla ya oparesheni ya vikosi maalum vya Marekani nchini Syria.
Baghdadi alijilipua na kujiua mwenyewe wakati wa oparesheni ya kumsaka.
Marekani imepuuza jukumu la vikosi vya Kikurdi katika oparesheni hiyo.
Akizungumzia oparesheni hiyo Oktoba 27, Rais wa Marekani Donald Trump alisema vikosi hivyo "vilisaidia" kutoa habari lakini akaongeza hawakufanya ''jukumu lolote la kijeshi".
Bwana Can alisisitiza kuwa SDF ilichangia sehemu muhimu ya oparesheni hiyo katika ujumbe wa twitter alioandika Jumatatu.
Ujuzi wote na ufikiaji wa al-Baghdadi na kitambulisho cha mahali pake kilikuwa ni matokeo ya kazi yetu wenyewe
"mchakato wote wa kiintelijensia wa kumtafuta al-Baghdadi na utambuzi wa mahali alipokuwa umetokana na juhudi zetu wenyewe. Maafisa wetu wa intelijensia walihusika katika mawasiliano na kutoa muongozo uliochangia kufaulu kwa oparesheni hiyo hadi dakika ya mwisho," alisema.
Bwana Can aliongeza kuwa SDF imekuwa ikifanya kazi CIA kumtafuta Baghdadi tangu Mei 15, na kwamba waligundua alikuwa akijificha katika mkoa wa Idlib, mahali ambako oparesheni hiyo ilitekelezwa.
Vyanzo vya habari vinasema Bwana Can, alibaini kuwa kiongozi huyo wa IS alikuwa karibu kuhamia eneo jingine mjini Jarablus.
SDF wamekuwa washirika muhimu wa Marekani katka mapambano dhidi ya kundi la Islamic State (IS), lakini mapema mwezi huu rais Trump aliwaondoa wanajeshi wa Marekani kaskazini mwa Syria.
Wachambuzi wanasema hatua ya Marekani kuondoa wanajeshi wake iliipatia nafasi Uturuki kuanzisha mashambulio ya mpakani katika eneo hilo.
Raisi Donald Trump amethibitisha kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa Operesheni hiyo pia imefanikiwa kumuua msaidizi namba moja wa al- Baghdad
Map of where the raid took place
Tunafahamu nini kuhusu oparasheni hiyo?
Washirika kadhaa wa Marekani au washirika wakuu katika eneo hilo waliarifiwa kuhusu oparesheni hiyo,ikiwemo Uturuki, Iraq, vikosi vya Kikurdi kaskazini mashariki mwa Syria, na Urusi, ambayo inadhibiti anga juu ya Idlib.
Rais Trump alisema kwamba vitengo vya ujasusi nchini Marekani vilimchunguza Baghdad kwa wiki kadhaa kabla ya operesheni na kwamba walijua eneo hilo lilikuwa na mahandaki kadhaa, huku mengi yakiwa na mwisho wake.
Siku ya Jumamosi, rais aliamrisha ujumbe uliohusisha kundi moja la wanajeshi maalum, ndege nane na meli nyingine nyingi.
Ndege aina ya helikopta iliyokuwa ikisafirisha kikosi maalum cha Marekani kiliondoka kutoka eneo ambalo halikutajwa baada mwendo wa saa kumi na moja saa za Marekani siku ya Jumamosi.
Ndege hizo zilipaa juu ya anga ya Uturuki, mbali na maeneo yanayodhibitiwa na majeshi ya Syria pamoja na yale ya Urusi.
Urusi ilishirikiana na kufungua anga yake kwa operesheni hiyo ya Marekani licha ya kutoambiwa kile kilichokuwa kikijiri kulingana na rais Trump.
''Operesheni hiyo ya kuingia na kutoka ilikuwa hatari mno. Kulikuwa na wakati ambapo tungekabiliwa vilivyo'' , alisema .
''Ndege zetu zilipaa chini chini lakini kwa mwendo wa kasi''.
Huku ndege hizo zikikaribia katika nyumba hiyo zilishambuliwa lakini Trump anasema mashambulizi hayo yalimalizwa haraka.
Wanajeshi walishuka kwa mashambulio makubwa ya risasi ardhini, ripoti zilisema.
Baada ya hapo vikosi vya Marekani vilimtaka Baghdadi, ambaye alikuwa amejificha ndani ya pango kutoka nje na kujisalimisha .
Abu Bakr al-Baghdadi akizungumza na wafuasi wake
Katika hutuba isiyo ya kawaida siku ya Jumapili , Rais Trump alisema Baghdadi alikufa baada ya kufika ukingoni alipokuwa akitoroka huko "akilia na kupiga mayowe wakati anafukuzwa na mbwa wa Marekani".
Baghdadi wakati huo alikuwa anatoroka akiandamana na watoto wake watatu wadogo ,lakini hatimae akajilipua kwa bomu alilokuwa amevaa baada ya kugundua kuwa amezingirwa.
Katika mlipuko huo Baghdadi na hao watoto wake wote watatu walifariki papohapo.
Rais Trump alisema japo mwili wa Baghdadi ulikuwa umechanika lakini waliweza kumtambua baada ya kuufanyia uchunguzi.
"Jambazi ambae alijitahidi sana kuwaogofya na kuwahangaisha wengine siku zake za mwisho alionekana mwenye mahangaiko,taharuki kubwa na kuchanganyikiwa ,alionekana mwenye uoga kupindukia alipogundua kikosi cha Marekani kilikuwa kinamkaribia , Rais Trump alisema.
Abu Bakr al-Baghdadi alijilipua wakati alipozingirwa na kikosi maalum cha Marekani.
Trump alisema matokeo ya uchunguzi uliofanyiwa maiti "ilitoa ishara malum, ambayo ilibaini moja kwa moja" kuwa ni Baghdadi.
Uchunguzi ulifanywa na wataalamu walioandamana na kikosi maalum katika eneo la tukio na walikuwa wamebeba sampuli ya chembe chembe za vinasaba DNA, ripoti ilisema.
Walitumia teknolojia mchanganyiko ya kutambua sura pamoja na mtambo mdogo wa kusoma matokeo ya DNA wakiwa ndani ya ndege kupata matokeo, kwa mujibu wa gazeti ya Daily Beast.
Wataalamu hao pia walibeba "kipande" cha mwili ili kuthibitisha matokeo ya uchunguzi wao.

Uganda: Wamiliki wa hoteli kuwasilisha taarifa za wateja polisi


Asan KasingyeHaki miliki ya picha
Image caption
Polisi nchini Uganda imetoa sera mpya ya usalama ambayo italazimu wamiliki na mameneja wa hoteli, vyumba vya wageni na maeneo mengine ya kulala kujulisha serikali kuhusu wageni wote ambao wanatumia maeneo yao.
Kulingana na sera hiyo mpya, orodha ya watu ambao wamelala kwenye hoteli yoyote, sasa itahitajika kupelekwa kwenye kituo cha polisi kilicho karibu kila asubuhi.
Asan Kasingye, afisa mwandamizi wa polisi anayesimamia polisi ya kijamii anasema orodha hizo zitawasaidia kujua kila anayeingia kwenye maeneo tofauti.
''Tunaamua kuandikisha kila mtu kwenye maeneo tofauti. Hata pia wale ambao wanalala na kutumia hoteli. Mamaneja wa hoteli hizi wanafaa kuandikisha watu wote na halafu watupe orodha hizi ili tuzitumie kwenye masuala ya usalama ," Kasingye alisema.
Kabla ya sera hiyo, wamiliki wa nyumba pekee ndiyo waliokuwa wanalazimishwa kupatia orodha ya wapangishaji wa nyumba zao. huwekwa na viongozi wa mitaa mbalimbali na nakala kupewa polisi.
Asan Kasingye, afisa mwandamizi wa polisi UgandaHaki miliki ya pichaUPD
Image caption''Tunaamua kuandikisha kila mtu kwenye maeneo tofauti. Hata pia wale ambao wanalala na kutumia hoteli.''
Polisi pia ilikuwa inafuatilia wateja wa kigeni wanaotembelea hoteli tofauti.
Lakini sasa, kila mteja ambaye jina lake litapatiwa polisi, atachunguzwa na maafisa wa upelelezi ili kujua historia yao ya uhalifu.
Hata hivyo chama la wamiliki wa hoteli nchini Uganda bado hakijajulishwa kirasmi kuhusu sera hii ya usalama, na wanasema wana mpango wa kukutana na kuzungumza kuhusu jinsi sera hii itakavyowaathiri.
''Tunahitaji kukutana kama wamiliki wa hoteli na kujaribu kuelewa sera hii. Sisi tunaunga mkono serikali kwa mambo ya usalama lakini tunachounga mkono haipaswi kuwa katika mgogoro na biashara yetu."Susan Muhwezi ni Mwenyekiti wa chama hicho alisema.
Sera hiyo mpya imezua gumzo miongoni mwa raia wa Uganda huku baadhi yao wakiunga mkono na wengine wakipinga.
Kwa miaka Zaidi ya kumi, polisi ya Uganda imekuwa ikijaribu mikakati tofauti ya usalama kukiwemo mkakati wa polisi ya kijami. Baadhi ya mikakati hiyo imefaulu, lakini ingine ikiwemo mkakati wa kundi la wananchi wanao zuia uhalifu haijafaulu.

Monday, October 28, 2019

Marubani wa Southwest Airlines: Walikuwa wakichukua filamu za moja kwa moja kutoka katika choo cha ndege hiyo


Rubani aliambia mfanyakazi wa ndege kwamba kamera hizo zilikuwa siri kubwa na mkakati wa kiusalamaHaki miliki ya picha
Image captio
Mfanyakazi wa kampuni ya ndege ya Southwest Airlines amewasilisha kesi mahakamani akiwashutumu marubani wawili kwa kuficha kamera katika choo cha ndege hiyo na kuwachukua picha za moja kwa moja abiria ambao walikuwa wakienda kujisaidia.
Renee Steinaker anadai kwamba aliwapata marubani hao wakati wa safari ya ndege ya mwaka 2017 kutoka Pittsburgh hadi Phoenix.
Rubani Terry Graham alimtaka kukaa katika chumba cha rubani na rubani mwenza Ryan Rusell, wakati alipotumia choo hicho, mashtaka hayo yanasema.
Rubani na kampuni ya ndege ya South West Arlines wamekana kwamba kulikuwa na kamera iliyokuwa ikiwachukua abiria na wafanyakazi waliokwenda msalani.
Kampuni hiyo imesema kwamba kisa hicho kilikuwa cha kushangaza.
Bi Steinaker anadai kwamba bwana Russell alimuonya kutosema kitu kuhusu kamera hiyo ambayo alisema ilikuwa mkakati wa usalama.
Mfanyakazi huyo aliripoti kisa hicho kwa kampuni hiyo, lakini anadai msimamizi mmoja alimuagiza kutomwambia mtu yeyote kilichotokea.
Marubani hao hawakuitwa na kampuni hiyo ya ndege na wanaendelea na kazi yao kawaida kulingana na mashtaka hayo.
''Madai yaliowasilishwa ni ya kikatili'', wakili anayemwakilisha bi Steinaker aliiambia BBC.

Je kampuni hiyo na marubani wake wamesema nini?

Katika taarifa kampuni ya ndege ya Southwest Airlines iliambia BBC kwamba kampuni hiyo haiweki kamera katika vyoo vya ndege.
Awali , kampuni hiyo ya ndege ya Marekani ilikataa kutoa tamko kuhusu kesi hiyo .
Lakini katika taarifa nyingine , ilisema imechunguza madai hayo na kupata kwamba hakukuwa hata na kamera moja katika choo.
Southwest itapinga mashtaka hayo , ilisema.
''Wakati kisa hicho kilipotokea siku mbili zilizopita, tulichunguza madai hayo na kuangazia hali hiyo na wafanyakazi waliohusika''.
Kisa hicho kimedaiwa kutokea wakati wa safari ya 2017 kutoka Pittsburgh hadi Phoenix
Kisa hicho kimedaiwa kutokea wakati wa safari ya 2017 kutoka Pittsburgh hadi PhoenixHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKisa hicho kimedaiwa kutokea wakati wa safari ya 2017 kutoka Pittsburgh hadi Phoenix
"Tunaweza kuthibitisha kutoka kwa uchunguzi wetu kwamba hakukuwa na kamera chooni, kisa hicho hakifai na kwamba kampuni hiyo haiwezi kukikubali''.
BBC imeomba tamko kutoka kwa mawakili wanowawakilisha marubani hao.
Katika majibu yao yalioandikwa kwa walalamishi bwana Russell na bi Graham walikiri kwamba kulikuwa na kipakatalishi katika chumba hicho cha marubani lakini walikana madai mengine yoyote, CNN iliripoti.

Je mashtaka hayo yanasemaje?

Saa mbili kabla ya safari ya ndege kuanza mnamo tarehe 27 Februari 2017, bi Graham alimuomba bi Stainaker kusalia katika chumba hicho cha marubani huku yeye akienda chooni , yalisema malalamishi hayo.
Kulingana na sera ya kampuni hiyo ya ndege wafanyakazi wawili wanafaa kuwepo katika chumba hicho cha ndege kila mara.
Bwana Russell alikiri kwamba kamera ilikuwa ikichukua watu moja kwa moja , huku akiwa na wasiwasi katika uso wake, kabla ya kumshauri bi Stainaker kutoambia mtu yeyote na kwamba ulikuwa mkakati wa kiusalama, yamesema malalamishi.
Kamera hizo zilikuwa na siri kubwa zikiwa zimewekwa katika kila ndege aina ya 737-800 , ilidaiwa kwamba bwana Graham alimwambia mfanyakazi mmoja wa ndege.
Na kufuatia maelezo ya bwana Russell, bi Stainaker alipiga picha ya kipakatalishi hicho na simu yake, yalisema mashtaka hayo.
Wakati bi Stainaker alipolalama, msimamizi mmoja alimwambia kunyamaza kuhusu suala hilo , na kwamba iwapo itajulikana hakuna mtu atakayesafiri kwa kutumia kampuni hiyo ya ndege.
Presentational grey line
Mashtaka hayo ya Bi Steinaker yanataka alipwe $50,000 kama fidia kutoka kwa kampuni ya Southwest Airlines pamoja na marubani.
Bwana Goldman alisema mteja wake alikua amedhurika na suala hiyo ambalo lilimsababishia dhiki kali.
Mashtaka hayo yaliwasilishwa katika kaunti ya Maricopa , jimbo la Arizona, lakini imehamishwa katika mahakama ya wilaya mjini Arizona.
Hakuna tarehe ya kusikilizwa kwa keshi hiyo imewekwa kufikia sasa.