Tuesday, October 29, 2019

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA


Baghdadi akihutubia wafuasi wake mjini Mosul mwaka 2014Haki miliki ya picha
Image caption
Vikosi vya muungano vya Syria (SDF) vinavyoongozwa na wapiganaji wa Kikurdi vinasema majasusi waliiba nguo za ndani za Abu Bakr al-Baghdadi ambayo ilitumiwa kufanya uchunguzi wa chembe chembe za vinasaba, DNA kabla auawe.
Kamanda wa mwandamizi wa SDF Polat Can anadai kuwa wapelelezi wao walichangia kwa kiasi kikubwa juhudi za kupata maficho ya kiongozi wa kundi la Islamic State (IS) kabla ya oparesheni ya vikosi maalum vya Marekani nchini Syria.
Baghdadi alijilipua na kujiua mwenyewe wakati wa oparesheni ya kumsaka.
Marekani imepuuza jukumu la vikosi vya Kikurdi katika oparesheni hiyo.
Akizungumzia oparesheni hiyo Oktoba 27, Rais wa Marekani Donald Trump alisema vikosi hivyo "vilisaidia" kutoa habari lakini akaongeza hawakufanya ''jukumu lolote la kijeshi".
Bwana Can alisisitiza kuwa SDF ilichangia sehemu muhimu ya oparesheni hiyo katika ujumbe wa twitter alioandika Jumatatu.
Ujuzi wote na ufikiaji wa al-Baghdadi na kitambulisho cha mahali pake kilikuwa ni matokeo ya kazi yetu wenyewe
"mchakato wote wa kiintelijensia wa kumtafuta al-Baghdadi na utambuzi wa mahali alipokuwa umetokana na juhudi zetu wenyewe. Maafisa wetu wa intelijensia walihusika katika mawasiliano na kutoa muongozo uliochangia kufaulu kwa oparesheni hiyo hadi dakika ya mwisho," alisema.
Bwana Can aliongeza kuwa SDF imekuwa ikifanya kazi CIA kumtafuta Baghdadi tangu Mei 15, na kwamba waligundua alikuwa akijificha katika mkoa wa Idlib, mahali ambako oparesheni hiyo ilitekelezwa.
Vyanzo vya habari vinasema Bwana Can, alibaini kuwa kiongozi huyo wa IS alikuwa karibu kuhamia eneo jingine mjini Jarablus.
SDF wamekuwa washirika muhimu wa Marekani katka mapambano dhidi ya kundi la Islamic State (IS), lakini mapema mwezi huu rais Trump aliwaondoa wanajeshi wa Marekani kaskazini mwa Syria.
Wachambuzi wanasema hatua ya Marekani kuondoa wanajeshi wake iliipatia nafasi Uturuki kuanzisha mashambulio ya mpakani katika eneo hilo.
Raisi Donald Trump amethibitisha kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa Operesheni hiyo pia imefanikiwa kumuua msaidizi namba moja wa al- Baghdad
Map of where the raid took place
Tunafahamu nini kuhusu oparasheni hiyo?
Washirika kadhaa wa Marekani au washirika wakuu katika eneo hilo waliarifiwa kuhusu oparesheni hiyo,ikiwemo Uturuki, Iraq, vikosi vya Kikurdi kaskazini mashariki mwa Syria, na Urusi, ambayo inadhibiti anga juu ya Idlib.
Rais Trump alisema kwamba vitengo vya ujasusi nchini Marekani vilimchunguza Baghdad kwa wiki kadhaa kabla ya operesheni na kwamba walijua eneo hilo lilikuwa na mahandaki kadhaa, huku mengi yakiwa na mwisho wake.
Siku ya Jumamosi, rais aliamrisha ujumbe uliohusisha kundi moja la wanajeshi maalum, ndege nane na meli nyingine nyingi.
Ndege aina ya helikopta iliyokuwa ikisafirisha kikosi maalum cha Marekani kiliondoka kutoka eneo ambalo halikutajwa baada mwendo wa saa kumi na moja saa za Marekani siku ya Jumamosi.
Ndege hizo zilipaa juu ya anga ya Uturuki, mbali na maeneo yanayodhibitiwa na majeshi ya Syria pamoja na yale ya Urusi.
Urusi ilishirikiana na kufungua anga yake kwa operesheni hiyo ya Marekani licha ya kutoambiwa kile kilichokuwa kikijiri kulingana na rais Trump.
''Operesheni hiyo ya kuingia na kutoka ilikuwa hatari mno. Kulikuwa na wakati ambapo tungekabiliwa vilivyo'' , alisema .
''Ndege zetu zilipaa chini chini lakini kwa mwendo wa kasi''.
Huku ndege hizo zikikaribia katika nyumba hiyo zilishambuliwa lakini Trump anasema mashambulizi hayo yalimalizwa haraka.
Wanajeshi walishuka kwa mashambulio makubwa ya risasi ardhini, ripoti zilisema.
Baada ya hapo vikosi vya Marekani vilimtaka Baghdadi, ambaye alikuwa amejificha ndani ya pango kutoka nje na kujisalimisha .
Abu Bakr al-Baghdadi akizungumza na wafuasi wake
Katika hutuba isiyo ya kawaida siku ya Jumapili , Rais Trump alisema Baghdadi alikufa baada ya kufika ukingoni alipokuwa akitoroka huko "akilia na kupiga mayowe wakati anafukuzwa na mbwa wa Marekani".
Baghdadi wakati huo alikuwa anatoroka akiandamana na watoto wake watatu wadogo ,lakini hatimae akajilipua kwa bomu alilokuwa amevaa baada ya kugundua kuwa amezingirwa.
Katika mlipuko huo Baghdadi na hao watoto wake wote watatu walifariki papohapo.
Rais Trump alisema japo mwili wa Baghdadi ulikuwa umechanika lakini waliweza kumtambua baada ya kuufanyia uchunguzi.
"Jambazi ambae alijitahidi sana kuwaogofya na kuwahangaisha wengine siku zake za mwisho alionekana mwenye mahangaiko,taharuki kubwa na kuchanganyikiwa ,alionekana mwenye uoga kupindukia alipogundua kikosi cha Marekani kilikuwa kinamkaribia , Rais Trump alisema.
Abu Bakr al-Baghdadi alijilipua wakati alipozingirwa na kikosi maalum cha Marekani.
Trump alisema matokeo ya uchunguzi uliofanyiwa maiti "ilitoa ishara malum, ambayo ilibaini moja kwa moja" kuwa ni Baghdadi.
Uchunguzi ulifanywa na wataalamu walioandamana na kikosi maalum katika eneo la tukio na walikuwa wamebeba sampuli ya chembe chembe za vinasaba DNA, ripoti ilisema.
Walitumia teknolojia mchanganyiko ya kutambua sura pamoja na mtambo mdogo wa kusoma matokeo ya DNA wakiwa ndani ya ndege kupata matokeo, kwa mujibu wa gazeti ya Daily Beast.
Wataalamu hao pia walibeba "kipande" cha mwili ili kuthibitisha matokeo ya uchunguzi wao.

Uganda: Wamiliki wa hoteli kuwasilisha taarifa za wateja polisi


Asan KasingyeHaki miliki ya picha
Image caption
Polisi nchini Uganda imetoa sera mpya ya usalama ambayo italazimu wamiliki na mameneja wa hoteli, vyumba vya wageni na maeneo mengine ya kulala kujulisha serikali kuhusu wageni wote ambao wanatumia maeneo yao.
Kulingana na sera hiyo mpya, orodha ya watu ambao wamelala kwenye hoteli yoyote, sasa itahitajika kupelekwa kwenye kituo cha polisi kilicho karibu kila asubuhi.
Asan Kasingye, afisa mwandamizi wa polisi anayesimamia polisi ya kijamii anasema orodha hizo zitawasaidia kujua kila anayeingia kwenye maeneo tofauti.
''Tunaamua kuandikisha kila mtu kwenye maeneo tofauti. Hata pia wale ambao wanalala na kutumia hoteli. Mamaneja wa hoteli hizi wanafaa kuandikisha watu wote na halafu watupe orodha hizi ili tuzitumie kwenye masuala ya usalama ," Kasingye alisema.
Kabla ya sera hiyo, wamiliki wa nyumba pekee ndiyo waliokuwa wanalazimishwa kupatia orodha ya wapangishaji wa nyumba zao. huwekwa na viongozi wa mitaa mbalimbali na nakala kupewa polisi.
Asan Kasingye, afisa mwandamizi wa polisi UgandaHaki miliki ya pichaUPD
Image caption''Tunaamua kuandikisha kila mtu kwenye maeneo tofauti. Hata pia wale ambao wanalala na kutumia hoteli.''
Polisi pia ilikuwa inafuatilia wateja wa kigeni wanaotembelea hoteli tofauti.
Lakini sasa, kila mteja ambaye jina lake litapatiwa polisi, atachunguzwa na maafisa wa upelelezi ili kujua historia yao ya uhalifu.
Hata hivyo chama la wamiliki wa hoteli nchini Uganda bado hakijajulishwa kirasmi kuhusu sera hii ya usalama, na wanasema wana mpango wa kukutana na kuzungumza kuhusu jinsi sera hii itakavyowaathiri.
''Tunahitaji kukutana kama wamiliki wa hoteli na kujaribu kuelewa sera hii. Sisi tunaunga mkono serikali kwa mambo ya usalama lakini tunachounga mkono haipaswi kuwa katika mgogoro na biashara yetu."Susan Muhwezi ni Mwenyekiti wa chama hicho alisema.
Sera hiyo mpya imezua gumzo miongoni mwa raia wa Uganda huku baadhi yao wakiunga mkono na wengine wakipinga.
Kwa miaka Zaidi ya kumi, polisi ya Uganda imekuwa ikijaribu mikakati tofauti ya usalama kukiwemo mkakati wa polisi ya kijami. Baadhi ya mikakati hiyo imefaulu, lakini ingine ikiwemo mkakati wa kundi la wananchi wanao zuia uhalifu haijafaulu.

Monday, October 28, 2019

Marubani wa Southwest Airlines: Walikuwa wakichukua filamu za moja kwa moja kutoka katika choo cha ndege hiyo


Rubani aliambia mfanyakazi wa ndege kwamba kamera hizo zilikuwa siri kubwa na mkakati wa kiusalamaHaki miliki ya picha
Image captio
Mfanyakazi wa kampuni ya ndege ya Southwest Airlines amewasilisha kesi mahakamani akiwashutumu marubani wawili kwa kuficha kamera katika choo cha ndege hiyo na kuwachukua picha za moja kwa moja abiria ambao walikuwa wakienda kujisaidia.
Renee Steinaker anadai kwamba aliwapata marubani hao wakati wa safari ya ndege ya mwaka 2017 kutoka Pittsburgh hadi Phoenix.
Rubani Terry Graham alimtaka kukaa katika chumba cha rubani na rubani mwenza Ryan Rusell, wakati alipotumia choo hicho, mashtaka hayo yanasema.
Rubani na kampuni ya ndege ya South West Arlines wamekana kwamba kulikuwa na kamera iliyokuwa ikiwachukua abiria na wafanyakazi waliokwenda msalani.
Kampuni hiyo imesema kwamba kisa hicho kilikuwa cha kushangaza.
Bi Steinaker anadai kwamba bwana Russell alimuonya kutosema kitu kuhusu kamera hiyo ambayo alisema ilikuwa mkakati wa usalama.
Mfanyakazi huyo aliripoti kisa hicho kwa kampuni hiyo, lakini anadai msimamizi mmoja alimuagiza kutomwambia mtu yeyote kilichotokea.
Marubani hao hawakuitwa na kampuni hiyo ya ndege na wanaendelea na kazi yao kawaida kulingana na mashtaka hayo.
''Madai yaliowasilishwa ni ya kikatili'', wakili anayemwakilisha bi Steinaker aliiambia BBC.

Je kampuni hiyo na marubani wake wamesema nini?

Katika taarifa kampuni ya ndege ya Southwest Airlines iliambia BBC kwamba kampuni hiyo haiweki kamera katika vyoo vya ndege.
Awali , kampuni hiyo ya ndege ya Marekani ilikataa kutoa tamko kuhusu kesi hiyo .
Lakini katika taarifa nyingine , ilisema imechunguza madai hayo na kupata kwamba hakukuwa hata na kamera moja katika choo.
Southwest itapinga mashtaka hayo , ilisema.
''Wakati kisa hicho kilipotokea siku mbili zilizopita, tulichunguza madai hayo na kuangazia hali hiyo na wafanyakazi waliohusika''.
Kisa hicho kimedaiwa kutokea wakati wa safari ya 2017 kutoka Pittsburgh hadi Phoenix
Kisa hicho kimedaiwa kutokea wakati wa safari ya 2017 kutoka Pittsburgh hadi PhoenixHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKisa hicho kimedaiwa kutokea wakati wa safari ya 2017 kutoka Pittsburgh hadi Phoenix
"Tunaweza kuthibitisha kutoka kwa uchunguzi wetu kwamba hakukuwa na kamera chooni, kisa hicho hakifai na kwamba kampuni hiyo haiwezi kukikubali''.
BBC imeomba tamko kutoka kwa mawakili wanowawakilisha marubani hao.
Katika majibu yao yalioandikwa kwa walalamishi bwana Russell na bi Graham walikiri kwamba kulikuwa na kipakatalishi katika chumba hicho cha marubani lakini walikana madai mengine yoyote, CNN iliripoti.

Je mashtaka hayo yanasemaje?

Saa mbili kabla ya safari ya ndege kuanza mnamo tarehe 27 Februari 2017, bi Graham alimuomba bi Stainaker kusalia katika chumba hicho cha marubani huku yeye akienda chooni , yalisema malalamishi hayo.
Kulingana na sera ya kampuni hiyo ya ndege wafanyakazi wawili wanafaa kuwepo katika chumba hicho cha ndege kila mara.
Bwana Russell alikiri kwamba kamera ilikuwa ikichukua watu moja kwa moja , huku akiwa na wasiwasi katika uso wake, kabla ya kumshauri bi Stainaker kutoambia mtu yeyote na kwamba ulikuwa mkakati wa kiusalama, yamesema malalamishi.
Kamera hizo zilikuwa na siri kubwa zikiwa zimewekwa katika kila ndege aina ya 737-800 , ilidaiwa kwamba bwana Graham alimwambia mfanyakazi mmoja wa ndege.
Na kufuatia maelezo ya bwana Russell, bi Stainaker alipiga picha ya kipakatalishi hicho na simu yake, yalisema mashtaka hayo.
Wakati bi Stainaker alipolalama, msimamizi mmoja alimwambia kunyamaza kuhusu suala hilo , na kwamba iwapo itajulikana hakuna mtu atakayesafiri kwa kutumia kampuni hiyo ya ndege.
Presentational grey line
Mashtaka hayo ya Bi Steinaker yanataka alipwe $50,000 kama fidia kutoka kwa kampuni ya Southwest Airlines pamoja na marubani.
Bwana Goldman alisema mteja wake alikua amedhurika na suala hiyo ambalo lilimsababishia dhiki kali.
Mashtaka hayo yaliwasilishwa katika kaunti ya Maricopa , jimbo la Arizona, lakini imehamishwa katika mahakama ya wilaya mjini Arizona.
Hakuna tarehe ya kusikilizwa kwa keshi hiyo imewekwa kufikia sasa.

Abu Bakr al-Baghdadi: Tunachokijua kuhusu uvamizi wa Marekani na mauaji yake Syria


Rais Trump akivihutubia vyombo vya habari kufutia kifo cha Baghdadi
Rais Donald Trump ametangaza kwamba kiongozi aliyekuwa akijificha wa kundi la Islamic State , Abu Bakr al Baghdad alijiuwa mwenyewe wakati wa uvamizi wa kikosi maalum cha Marekani nchini Syria.
Hiki ndicho tunachojua kuhusu operesheni hiyo.

Ni wapi na lini ilitekelezwa?

Katika tangazo la runinga , bwana Trump alitangaza kwamba gaidi huyo nambari moja duniani amefariki wakati wa uvamizi hatari wa usiku kaskazini magharibi mwa Syria na vikosi maalum vya Marekani.
Marekani ilikuwa imetoa kitita cha dola milioni 25 kwa habari kuhusu alipo Abu bakr al BaghdadiHaki miliki ya pichaAFP
Image captionMarekani ilikuwa imetoa kitita cha dola milioni 25 kwa habari kuhusu alipo Abu bakr al Baghdadi
Rais alisema kwamba ndege aina ya helikopta iliokisafirisha kikosi hicho maalum iliondoka kutoka eneo ambalo halikutajwa baada mwendo wa saa kumi na moja saa za Marekani siku ya Jumamosi, wakati yeye na viongozi wengine walikusanyika katika chumba cha Ikulu ya Whitehouse.
Ndege zilisafiri kwa muda wa saa moja na dakika 10 kutoka maeneo tofauti, hiuku opetresheni ya ardhini ikifanyika kwa muda wa saa mbili, aliongezea.
Maafisa waliambia vyombo vya habari nchini Marekani kwamba mapema siku ya Jumapili nchini Syria, vikosi maalum vya Marekani vililenga eneo moja la kijiji cha Barisha mkoani Idlib takriban kilomita 5 kusini mwa mpaka wa Uturuki.
Eneo alilokuwa kiongozi huyo wa Islamic State Syria
Presentational white space
Idlib ndio ngome ya mwisho ya upinzani dhidi ya serikali ya Bashar al Asad.
Inatawaliwa na muungano wa wapiganaji wa Jihad ambao unakinzana na Kundi la Islamic State , lakini mamia ya wapiganaji wa IS wanaaminika kupiga kambi katika eneo hilo.
Jeshi la Syria linaloungwa mkono na Syria lipo mashariki, magharibi na kusini.

Jinsi uvamizi huo ulivyofanyika

Bwana Trump alisema kwamba vitengo vya ujasusi nchini Marekani vilimchunguza Baghdad kwa wiki kadhaa kabla ya operesheni na kwamba walijua eneo hilo lilikuwa na mahandaki kadhaa, huku mengi yakiwa na mwisho wake.
Siku ya Jumamosi , rais aliamrisha ujumbe uliohusisha kundi moja la wanajeshi maalum , ndege nane na meli nyingine nyingi.
Picha zikimuonyesha rais donld Trump na viongozi wengine wa kisiasa na kijeshi wakiwa katika chumba kimoja cha Ikulu ya Whitehouse
Ndege hizo zilipaa juu ya anga ya Uturuki, mbali na maeneo yanayodhibitiwa na majeshi ya Syria pamoja na yale ya Urusi.
Urusi ilishirikiana na kufungua nga yake kwa operesheni hiyo ya Marekani licha ya kutoambiwa kile kilichokuwa kikijiri kulingana na rais Trump.
''Operesheni hiyo ya kuingia na kutoka ilikuwa hatari mno. Kulikuwa na wakati ambapo tungekabiliwa vilivyo'' , alisema .
''Ndege zetu zilipaa chini chini lakini kwa mwendo wa kasi''.
Huku ndege hizo zikikaribia katika nyumba hiyo zilishambuliwa lakini Trump anasema mashambulizi hayo yalimalizwa haraka.
Mkaazi mmoja wa Barisha anasema kwamba ndege hizo za Marekani zilishambulia nyumba mbili na kuiharibu kabisa mojaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionMkaazi mmoja wa Barisha anasema kwamba ndege hizo za Marekani zilishambulia nyumba mbili na kuiharibu kabisa moja
Mwanakiji mmoja kutoka eneo la Barisha aliambia BBC kulikuwa na mashambulizi kutoka kwa helikopta hizo kwa zaidi ya dakika 30 kabla ya vikosi vya ardhini kuingia eneo hilo, akiongezea kwamba ndege hizo zilishambulia nyumba mbili na kuiharibu kabisa mojawapo.
Baada ya ndege hizo kutua , wanajeshi hao maalum walilipua mashimo katika kuta ya nyumba hizo ili kukwepa kuingia ndani kupitia mlango wa mbele uliowekwa vilipuzi na baadaye kuanza kuondoa vifusi kulingana na Trump.

Unaweza pia kusoma:

Rais huyo alisema kwamba Baghdad alifariki baada ya kutorokea katika handaki lililo na mwisho, akilia na kupiga kelele.
Hakuna uthibtisho huru wa mauaji ya BaghdadiHaki miliki ya pichaAFP
Image captionHakuna uthibtisho huru wa mauaji ya Baghdadi
Watoto 11 waliondolewa katika nyumba hiyo bila majeraha kufikia wakati huo, huku watu wakisalimu amri na wengine kupigwa risasi.
''Aliyekuwa amesalia alikuwa Baghdadi pekee katika handaki pamoja na watoto watatu'', aliongezea.
''Alifika mwisho wa handaki , huku mbwa wetu wakimfukuza . Alikuwa ameweka vilipuzi katika nguo yake ya ndani na akajilipua na watoto hao watatu''.
''Mwili wake ulikatwakatwa na mlipuko huo huku handaki hilo likiuangukia'' , aliongezea.
Picha na kanda za video kuhusu kilichotokea baada ya uvamizi huo wa Marekani zilionyesha vifusi vya jengo lililoharibiwa pamoja na gari lililochomeka likiwa na mashimo chungu nzima ya risasi.

Kwa nini Marekani ina hakika Baghdadi amefariki?

Bwana Trump amesema kuwa matokeo ya vipimo vya mabaki ya mtu aliyejilipua katika handaki hilo yalionyesha kwamba alikuwa Baghdadi.
Ilichukua takriban muda wa dakika 15 baada ya kufariki.
''Vipimo hivyo vilifanywa na wataalam waliosafiri na vikosi hivyo maalum na walikuwa na sampuli ya vinasaba vya Baghdadi'', aliongezea.
Wataalam hao pia walibeba vipande vya mabaki ya mwili wake katika ndege hizo, kulingana na Trump. Hakujakuwa na uthibitisho huru kuhusu kifo cha Baghdad. Wafuasi wa IS wamekuwa wakionyana kuhusu kuamini tangazo hilo la Marekani.

Je kuna majeraha mengine?

Rais huyo alisema: hakuna hata mwanajeshi ama afisa mmoja wa Marekani aliyeuawa katika operesheni hoyo, huku idadi kubwa ya wapiganaji wa Baghdadi na washirika wao wakifariki naye.
Chombo cha habari cha Jihadi mjini Idlib lkimesema kwamba basi la raia lilishambuliwaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionChombo cha habari cha Jihadi mjini Idlib lkimesema kwamba basi la raia lilishambuliwa
Wake wawili wa Baghdadi ni miongoni mwa waliokufa
Bwana Trump anasema kwamba wanawake hao walipatikana wakiwa wamevalia fulana za ndani zilizowekwa vilipuzi ambavyo havikulipuliwa.
Mbwa wa Marekani alijeruhiwa katika handaki hilo mahala ambapo Baghdadi alifariki , kulingana na Trump .
Haijajulikani iwapo wafuasi wa IS ama watoto waliokamatwa walijeruhiwa.
Bwana Trump alisema kwamba wapiganaji hao kwa sasa wanazuiliwa huku watoto hao wakiwekwa chini ya usimamizi wa mtu ambaye hakutajwa.

Kwa nini Baghdadi alijificha Idlib?

Mji wa Barisha upo mamia ya kilomita kutoka eneo la jangwa lililo mashambani katika mpaka wa Syria na Iraq ambapo Baghdadi aliaminika kujificha.
Bwana Trump alisema kwamba, Baghdadi alikuwa Idlib kwa kuwa alikuwa na lengo la kujenga upya jeshi lake la wapiganaji wa IS baada ya vikosi vya Kikurdi vinvyoongozwa na Marekani kuteka ngome zake za mwisho zilizosalia karibu na kijiji cha Baghuz kilicho mashariki mwa Syria mwezi Machi.
''Hiyo ndio sababu iliomfanya kusalia katika eneo hilo'', rais huyo aliongezea. Hilo ndio eneo muhimu unapozungumzia kujenga upya kundi hilo.
Anasema kwamba ripoti muhimu za kijasusi kuhusu mipango ya siku zijazo ya Baghdadi ilipatikana wakati wa shambulio hilo na kwamba Marekani itamsaka yeyote yule atakayemrithi.
''Tunawajua watakaomrithi. Na tayari tumeanza kuwaaangazia''.

Je Abu Bakr al-Baghdadi ni nani?

Alizaliwa 1971 katika eneo la Samarra nchini Iraq.
Akiwa angali mtoto alidaiwa kupenda sama kusoma Quran na kufuata sheria za kidini, akiwalaumu ndugu zake wasiofutwa vizuri dini ya Kiislamu.
Lakini ilikuwa wakati ambapo alikuwa anafuzu kupata Stashahada ya somo la Quran katika chuo kikuu cha Saddam Husein , ndio wakati alijihusisha na msimamo mkali wa kundi hilo.
Mwisho wa mwaka 2000 alikuwa ameanzisha kundi linalofuata sunna na aliendelea hadi kushirikishwa na kundi la al-qaeda nchini Iraq ambapo kundi la Islamic state lilibuniwa.
Tangu 2014 amesalia mkimya kwa muda mrefu huku kukiwa na uvumi wa kifo chake ambao haujathibitishwa.